Balozi Dkt. Elsie S. Kanza Afanya Ziara Dallas, Texas
- Leo Nzali

- Mar 8
- 1 min read
Updated: Mar 13

Katika ziara hiyo, Balozi Kanza alizindua rasmi Nevet Counseling Center, kituo cha ushauri na tiba ya afya ya akili kilichopo ndani ya jengo la Holy Cross Lutheran Church. Kituo hicho kinamilikiwa na Deborah Mwamgomo LPC-A na kinalenga kutoa huduma za ushauri wa afya ya akili kwa Watanzania na jamii pana ya Waafrika wanaoishi Texas.
Akizungumza na The Diaspora Magazine, Bi. Mwamgomo alisema kituo hicho kitasaidia kukabiliana na changamoto za maisha ya ughaibuni kwa kutoa ushauri wa kitaalamu unaozingatia pia mila na utamaduni wa Kitanzania.

Katika hafla hiyo pia, Balozi Dkt. Kanza alisaini kitabu kipya cha Mental Health and Parenting in Diaspora kilichoandikwa na Deborah Mwamgomo, kinachozungumzia afya ya akili na malezi kwa familia zinazoishi nje ya nchi(ughaibuni).
Aidha, Balozi Kanza alikuwa mgeni rasmi katika Kongamano la 12 la Umoja International Prayerline na alipata fursa ya kukutana na kuzungumza na Watanzania wanaoishi Dallas kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu huduma za ubalozi wa Tanzania nchini Marekani. 🇹🇿











Comments